*SABABU 11 ZA UONGO ZINAZOTUMIWA NA WANADAMU KUHAFIFISHA SABATO*

*SABABU 11 ZA UONGO ZINAZOTUMIWA NA WANADAMU KUHAFIFISHA SABATO*

Bwana asifiwe mpendwa Msomaji wangu, nimekuwa nikitoa masomo mengi kwa habari ya Sabato.

basi kwa siku ya leo tutazichunguza kama zinae UKWELI wowote juu ya hili

sababu 11 watu waznazodai ya kwamba Sabato ilibadilishwa

*1. Je,  tuheshimu  Jumapili  kwa  kuwa  Yesu  alifufuka  siku  hiyo?*_ _Hapana._ 

Ni  kweli  baadhi  ya  wakristo  wa  awali  kwenye  miaka  ya  90  hadi  100  BK  walichagua kupumzika    Jumapili    kuepuka    mateso    makali    yaliyowatofautisha    na    watu    wengine.   

Hata hivyo  Yesu  anadai  Je,  tukatae  amri  ya  Mungu  kwa  kuheshimu  mapokeo?  Wanafunzi waliokutana  Jumapili  wengi  hawakuamini kama Yesu  amefufuka _(Mk. 16:12-14)._ Zaidi ya yote, mkutano  wao  wa  Jumapili  ulikuwa  kwa  hofu  ya  Wayahudi  _(Yoh.  20:19)._ 

Yako  maadhimisho mengine muhimu kama ubatizo na meza ya Bwana je na hayo tuyawekee siku gani?

*2.  Je,  si  kalenda  imebadilishwa?*

_Ni  kweli  kalenda  ilibadilishwa  mwaka  1582  lakini  haikuingilia  mzunguko  wa  juma  lenye  siku saba._

πŸ‘† Kilichobadilishwa  na  Papa  Gregory  XIII  kilikuwa  kusahihisha  kosa  kwenye  kalenda  ya Julian  *(46  BC)*  iliyosema  mwaka  una  siku  *365¼.*    Kwa  uhalisia  kuna  dakika  11  pungufu  katika hesabu  hiyo.  Hadi  mwaka  *1582* ,  kulikuwa  na  upungufu  wa  siku  10.  Hivyo,  mwaka  *1582* kulikucha  Alhamisi  4  Oktoba  *1582*  na  kesho  yake  kukawa  Ijumaa  tarehe  *15*  Oktoba  *1582* .

_Tunapoabudu siku ya sabato tunafanya kama Yesu alivyoabudu._ *(Luka 4:16.)*

*3.  Ni vigumu  kutambua ni  siku  ipi  ndiyo  ya  saba  katika  wiki.*

    _Ziko  sababu  mbili  kuhusiana  na  jambo  hili._ 

Kwanza  ni  siku  aliyokufa  Yesu  *Luka  23:52-56* kwamba    alikufa    Ijumaa    na    alifufuka    Jumapili.  *(Luka    24:1 – 2).*

   Pili    ni  majina    ya    siku  ya Jumamosi  katika  lugha  mbali  mbali  zaidi  ya  100  bado  ni  sabato.

πŸ‘†  Italia,  siku  ya  Jumamosi  ni Sabbato,  Hispania  ni  Sabado,  Ureno  ni  Sabbado,  Urusi  ni  Subbota,  Poland  ni  Sobota  na Ugiriki  ni  Sabbatho. 

Maana  ya  majina  yote  hayo  ni  kwamba  Jumamosi  ndiyo  sabato.

πŸ‘† Ikiwepo hoja  ya  tatu  basi  ni  Kamusi.  Ukisoma  Kamusi,  neno  sabato,  ni  siku  ya  saba  ya  juma  kwetu  ni Jumamosi.

*4. Je  naweza  kutunza  siku  yoyote  katika  juma  na  kuiita  Sabato?* _La:_

_Law.  10:1-2._  Wana  wa  Haruni  walipoleta  moto  wa  kigeni  kwenye  madhabahu, waliangamizwa  papo  hapo.

Hivyo,  ni  lazima  kutakasa  siku  aliyoiweka  Bwana  mwenyewe. *(Kut. 20:  10.)*  Zaidi  ya  yote,  ukivunja  amri  moja,  umekosa  juu  ya  yote.
(somaπŸ‘‰ *Yak.  2:10.*

Kwa  miaka 40  yaani  zaidi  ya  sabato  2000,  Mungu  aliwafundisha  Israeli  Sabato.  (Kut.  16.)  Kuokota  siku  6, sabato hakipatikani na Ijumaa kiliokotwa kikahifadhiwa pasipo kuharibika. 5.      Tutaitakasa  siku  ya  Bwana,  achana  na  Sabato  *Ufunuo  1:9, 10*    hutambulisha    siku    ya    Bwana.
    Siku    za    Bwana    ziko    nyingi.    Malaki    4:1,    5 husema  juu  ya  aina  mojawapo  na  *Isaya  58:13*  husema  juu  ya  Sabato.
  Yesu  alisema  ndiye Bwana  wa  Sabato.  *(Mk.  2:28.).*  Siku  ya  sabato  humtambulisha  Mungu  kuwa  Muumbaji  na mkombozi  na  ndio  maana  uzito  umewekwa  kwamba  tuikumbuke  siku  ya  sabato  tuitakase. (Kut.20:8).

*6. Sabato  ilifanyika  kwa  ajili  ya  Wayahudi  peke  yao.*

πŸ‘† _Kuna  uwongo  wa  kutisha  ulioenea  duniani  kwamba  sabato  ni  ya  Wayahudi._  Lakini  ndani  ya Biblia  wazo  hilo  haliungwi  mkono.

Sabato  inayoungwa  mkono,  ni  _sabato  ya  Bwana._  *Kut. 20:10,*  Ni  kweli  lipo  sinagogi  la  Wayahudi.  (  Mdo10:22,  12:11,  10:39  na  14:1.)  Lakini  sabato  ni ya Bwana  Kut.  20:10,  Sabato  ilifanyika  kwa  ajili  ya  mwanadamu  πŸ‘‰ *Mk.  2:27.*

_Hivyo, kila aliye mwanadamu, sabato ni kwa ajili yake._

Luka ambaye hakuwa myahudi alitakasa sabato *(Mdo. 16:13.)* Na waongofu waliabudu siku ya Sabato *(Mdo. 14:42 – 44).*

  *7.   Amri 10 zilibatilishwa ikiwemo sabato.*

_Inaumiza moyo kwamba wako watu wanaolisema jambo hili pasipo kuungwa mkono na Maandiko Matakatifu._

Paulo anasema, kama isingekuwapo sheria, pasingekuwa na dhambi wala kusingekuwepo haja ya mwokozi. *Rum. 4:15.*

πŸ‘†Sheria ya Mungu yote, pamoja na sabato ni ya haki, takatifu na njema

*Rum. 7:12.* _Sheria ya Mungu huwakilisha tabia ya Mungu._

*SHERIA ZA MUNGU  NA NI MWAKISIO WA TABIA YA MUNGU* 

*Rum 16:26  Mungu wa milele*

Zab. 111: 7,8  _Sheria ni ya milele_

*Luk.18:19  Mungu ni mwema*

_Rum. 7:12   Sheria ni njema_

*Yoh. 4:24  Mungu ni wa kiroho*

Rum.7:14  _Sheria ni ya kiroho_

*Kumb. 32:4  Mungu ni wa haki*

Rum. 7:12   _Sheria ni ya haki_

*Zab. 145:17 Mungu ni wa haki*

Zab.119:172  _Sheria ni ya haki_

*1 Yoh. 3:3  Mungu ni safi*
        
_Zab. 19:8  Sheria ni safi_

*Mt. 5:48* _*Mungu ni mkamilifu*_

*Zab. 19:7* _Sheria ni kamilifu_

*1Yoh. 4:8* *Mungu ni pendo*

Rum. 13:10 _Sheria ni pendo_

1 Yoh. 1:5 Mungu ni nuru

Mith. 6:23 Sheria ni nuru

Zab. 48:1 Mungu ni mkuu

Hos. 8:12 Sheria ni kuu

Kumb. 32:4 Mungu ni Kweli

Zab. 119:142 Sheria ni kweli

Isa. 5:16 Mungu ni mtakatifu

Rum. 7:12 Sheria ni takatifu


Kwa kuwa sheria ya Mungu ni mwakisio wa tabia ya Mungu, kwa kadiri tabia ya Mungu isivyobadilika,  basi  sheria  nayo  haitabadilika.

Kama  ingekuwa  rahisi  Mungu  kubadilisha sheria yake, basi asingekubali Yesu kuja kufa msalabani kwa ajili ya wanadamu.

Juu ya sheria ya Mungu  kutofautiana na kile kinachoitwa Sheria ya Musa,

Angalia somo la Sheria ya Mungu. 

8.   Sabato ilibatilishwa Ni kweli yako mafungu ya Biblia yanayosema sabato ilibatilishwa.
(Kol. 2:16, Gal. 4:10 and Rum 14:5)

  Biblia ikisomwa kwa makini itafunua kwamba hizi ni sabato zinazohusiana na sikukuu.

Kufuatana na Mambo ya _Walawi sura ya 23:_ angalia hasa fungu la 37, 38 kwamba zilitolewa kama nyongeza na ndio maana Paulo alizipinga. Tofauti na Sabato ya siku ya Saba, hiyo  ilikuwapo  kabla  ya  dhambi

  (Mwa.2:1-3).  Mungu  akaiweka  kwenye  sheria  yake  ya maadili yaani amri kumi (Kut.20:8-11). Ni alama ya Mungu kwa aliowaumba na kuwatakasa (Kut.31:17, 13; Eze.20:20, 12).

Yesu alipokuwako duniani aliiheshimu. (Luk.4:16, Mt.24:20) na kwa kuwa Kristo habadiliki (Ebr.13;8), itakuwa furaha yake watakatifu kuabudu mbele zake siku za sabato, kwenye mbingu mpya na nchi mpya. (Isa.66:22, 23).

*9.   Tuko chini ya neema hivyo hatulazimiki kutii sheria.*

*Rum. 6:14 – 15* _, Paulo anasema kwamba kwa kuwa chini ya neema, hatubatilishi sheria (Rum. 3: 31, Rum. 3:20.)_

*10. Tukiwa ndani ya Kristo, pumziko linatosha hivyo hatuihitaji sabato.*

_Ni Mungu ndiye atoaye raha hata kwa kupitia sabato yake. “Iko raha ya sabato kwa watu wa Mungu” (Ebr. 4:1-5, 9, 10)._

*N:B*
  _Jinsi wokovu ulivyo muhimu kwa mwanadamu, *(Yoh. 3;16)* ndivyo sabato ilivyo muhimu kwa wanadamu. *(Mk.2:27)*_


*11.  Watu  wengi  hawawezi  kuwa wamekosea Wingi  si  hoja,  bali  ubora  wa  tabia  ndio  Mungu  anaoutaka.*

  *(Mt.  7:  13,  14).*  _Izingatiwe  pia kwamba    ilionywa    kuwa    watazuka    watu    wenye    kufundisha    kwa    kufuata    tamaa    zao._  

*(2 Timothy 4:3).* Kwa hiyo kwa wingi wao, wanadamu wanaweza kukosea.

Namna ya Kuikumbuka  Sabato  na  Kuitakasa Kukumbuka  na  kuitakasa  sabato  ni  kuelewa  na  kutekeleza  kile  ambacho  Mungu  anataka  juu ya siku yake.

Mungu hajatuacha juu ya mwongozo kwa jambo hili.

SOMO lijalo tutajifunza kwa habari namna ya kuitunza Sabato

kupata masomo kama haya tembelea blog yangu inaitwa
πŸ‘‡
https://masalianautume255.blogspot.com

MUNGU AKUBARIKI

0627729770(sms or call)

0712336509(whatsap)

__________Isack Mussa______

Comments