*SABABU 11 ZA UONGO ZINAZOTUMIWA NA WANADAMU KUHAFIFISHA SABATO*
Bwana asifiwe mpendwa Msomaji wangu, nimekuwa nikitoa masomo mengi kwa habari ya Sabato.
basi kwa siku ya leo tutazichunguza kama zinae UKWELI wowote juu ya hili
sababu 11 watu waznazodai ya kwamba Sabato ilibadilishwa
*1. Je, tuheshimu Jumapili kwa kuwa Yesu alifufuka siku hiyo?*_ _Hapana._
Ni kweli baadhi ya wakristo wa awali kwenye miaka ya 90 hadi 100 BK walichagua kupumzika Jumapili kuepuka mateso makali yaliyowatofautisha na watu wengine.
Hata hivyo Yesu anadai Je, tukatae amri ya Mungu kwa kuheshimu mapokeo? Wanafunzi waliokutana Jumapili wengi hawakuamini kama Yesu amefufuka _(Mk. 16:12-14)._ Zaidi ya yote, mkutano wao wa Jumapili ulikuwa kwa hofu ya Wayahudi _(Yoh. 20:19)._
Yako maadhimisho mengine muhimu kama ubatizo na meza ya Bwana je na hayo tuyawekee siku gani?
*2. Je, si kalenda imebadilishwa?*
_Ni kweli kalenda ilibadilishwa mwaka 1582 lakini haikuingilia mzunguko wa juma lenye siku saba._
π Kilichobadilishwa na Papa Gregory XIII kilikuwa kusahihisha kosa kwenye kalenda ya Julian *(46 BC)* iliyosema mwaka una siku *365¼.* Kwa uhalisia kuna dakika 11 pungufu katika hesabu hiyo. Hadi mwaka *1582* , kulikuwa na upungufu wa siku 10. Hivyo, mwaka *1582* kulikucha Alhamisi 4 Oktoba *1582* na kesho yake kukawa Ijumaa tarehe *15* Oktoba *1582* .
_Tunapoabudu siku ya sabato tunafanya kama Yesu alivyoabudu._ *(Luka 4:16.)*
*3. Ni vigumu kutambua ni siku ipi ndiyo ya saba katika wiki.*
_Ziko sababu mbili kuhusiana na jambo hili._
Kwanza ni siku aliyokufa Yesu *Luka 23:52-56* kwamba alikufa Ijumaa na alifufuka Jumapili. *(Luka 24:1 – 2).*
Pili ni majina ya siku ya Jumamosi katika lugha mbali mbali zaidi ya 100 bado ni sabato.
π Italia, siku ya Jumamosi ni Sabbato, Hispania ni Sabado, Ureno ni Sabbado, Urusi ni Subbota, Poland ni Sobota na Ugiriki ni Sabbatho.
Maana ya majina yote hayo ni kwamba Jumamosi ndiyo sabato.
π Ikiwepo hoja ya tatu basi ni Kamusi. Ukisoma Kamusi, neno sabato, ni siku ya saba ya juma kwetu ni Jumamosi.
*4. Je naweza kutunza siku yoyote katika juma na kuiita Sabato?* _La:_
_Law. 10:1-2._ Wana wa Haruni walipoleta moto wa kigeni kwenye madhabahu, waliangamizwa papo hapo.
Hivyo, ni lazima kutakasa siku aliyoiweka Bwana mwenyewe. *(Kut. 20: 10.)* Zaidi ya yote, ukivunja amri moja, umekosa juu ya yote.
(somaπ *Yak. 2:10.*
Kwa miaka 40 yaani zaidi ya sabato 2000, Mungu aliwafundisha Israeli Sabato. (Kut. 16.) Kuokota siku 6, sabato hakipatikani na Ijumaa kiliokotwa kikahifadhiwa pasipo kuharibika. 5. Tutaitakasa siku ya Bwana, achana na Sabato *Ufunuo 1:9, 10* hutambulisha siku ya Bwana.
Siku za Bwana ziko nyingi. Malaki 4:1, 5 husema juu ya aina mojawapo na *Isaya 58:13* husema juu ya Sabato.
Yesu alisema ndiye Bwana wa Sabato. *(Mk. 2:28.).* Siku ya sabato humtambulisha Mungu kuwa Muumbaji na mkombozi na ndio maana uzito umewekwa kwamba tuikumbuke siku ya sabato tuitakase. (Kut.20:8).
*6. Sabato ilifanyika kwa ajili ya Wayahudi peke yao.*
π _Kuna uwongo wa kutisha ulioenea duniani kwamba sabato ni ya Wayahudi._ Lakini ndani ya Biblia wazo hilo haliungwi mkono.
Sabato inayoungwa mkono, ni _sabato ya Bwana._ *Kut. 20:10,* Ni kweli lipo sinagogi la Wayahudi. ( Mdo10:22, 12:11, 10:39 na 14:1.) Lakini sabato ni ya Bwana Kut. 20:10, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu π *Mk. 2:27.*
_Hivyo, kila aliye mwanadamu, sabato ni kwa ajili yake._
Luka ambaye hakuwa myahudi alitakasa sabato *(Mdo. 16:13.)* Na waongofu waliabudu siku ya Sabato *(Mdo. 14:42 – 44).*
*7. Amri 10 zilibatilishwa ikiwemo sabato.*
_Inaumiza moyo kwamba wako watu wanaolisema jambo hili pasipo kuungwa mkono na Maandiko Matakatifu._
Paulo anasema, kama isingekuwapo sheria, pasingekuwa na dhambi wala kusingekuwepo haja ya mwokozi. *Rum. 4:15.*
πSheria ya Mungu yote, pamoja na sabato ni ya haki, takatifu na njema
*Rum. 7:12.* _Sheria ya Mungu huwakilisha tabia ya Mungu._
*SHERIA ZA MUNGU NA NI MWAKISIO WA TABIA YA MUNGU*
*Rum 16:26 Mungu wa milele*
Zab. 111: 7,8 _Sheria ni ya milele_
*Luk.18:19 Mungu ni mwema*
_Rum. 7:12 Sheria ni njema_
*Yoh. 4:24 Mungu ni wa kiroho*
Rum.7:14 _Sheria ni ya kiroho_
*Kumb. 32:4 Mungu ni wa haki*
Rum. 7:12 _Sheria ni ya haki_
*Zab. 145:17 Mungu ni wa haki*
Zab.119:172 _Sheria ni ya haki_
*1 Yoh. 3:3 Mungu ni safi*
_Zab. 19:8 Sheria ni safi_
*Mt. 5:48* _*Mungu ni mkamilifu*_
*Zab. 19:7* _Sheria ni kamilifu_
*1Yoh. 4:8* *Mungu ni pendo*
Rum. 13:10 _Sheria ni pendo_
1 Yoh. 1:5 Mungu ni nuru
Mith. 6:23 Sheria ni nuru
Zab. 48:1 Mungu ni mkuu
Hos. 8:12 Sheria ni kuu
Kumb. 32:4 Mungu ni Kweli
Zab. 119:142 Sheria ni kweli
Isa. 5:16 Mungu ni mtakatifu
Rum. 7:12 Sheria ni takatifu
Kwa kuwa sheria ya Mungu ni mwakisio wa tabia ya Mungu, kwa kadiri tabia ya Mungu isivyobadilika, basi sheria nayo haitabadilika.
Kama ingekuwa rahisi Mungu kubadilisha sheria yake, basi asingekubali Yesu kuja kufa msalabani kwa ajili ya wanadamu.
Juu ya sheria ya Mungu kutofautiana na kile kinachoitwa Sheria ya Musa,
Angalia somo la Sheria ya Mungu.
8. Sabato ilibatilishwa Ni kweli yako mafungu ya Biblia yanayosema sabato ilibatilishwa.
(Kol. 2:16, Gal. 4:10 and Rum 14:5)
Biblia ikisomwa kwa makini itafunua kwamba hizi ni sabato zinazohusiana na sikukuu.
Kufuatana na Mambo ya _Walawi sura ya 23:_ angalia hasa fungu la 37, 38 kwamba zilitolewa kama nyongeza na ndio maana Paulo alizipinga. Tofauti na Sabato ya siku ya Saba, hiyo ilikuwapo kabla ya dhambi
(Mwa.2:1-3). Mungu akaiweka kwenye sheria yake ya maadili yaani amri kumi (Kut.20:8-11). Ni alama ya Mungu kwa aliowaumba na kuwatakasa (Kut.31:17, 13; Eze.20:20, 12).
Yesu alipokuwako duniani aliiheshimu. (Luk.4:16, Mt.24:20) na kwa kuwa Kristo habadiliki (Ebr.13;8), itakuwa furaha yake watakatifu kuabudu mbele zake siku za sabato, kwenye mbingu mpya na nchi mpya. (Isa.66:22, 23).
*9. Tuko chini ya neema hivyo hatulazimiki kutii sheria.*
*Rum. 6:14 – 15* _, Paulo anasema kwamba kwa kuwa chini ya neema, hatubatilishi sheria (Rum. 3: 31, Rum. 3:20.)_
*10. Tukiwa ndani ya Kristo, pumziko linatosha hivyo hatuihitaji sabato.*
_Ni Mungu ndiye atoaye raha hata kwa kupitia sabato yake. “Iko raha ya sabato kwa watu wa Mungu” (Ebr. 4:1-5, 9, 10)._
*N:B*
_Jinsi wokovu ulivyo muhimu kwa mwanadamu, *(Yoh. 3;16)* ndivyo sabato ilivyo muhimu kwa wanadamu. *(Mk.2:27)*_
*11. Watu wengi hawawezi kuwa wamekosea Wingi si hoja, bali ubora wa tabia ndio Mungu anaoutaka.*
*(Mt. 7: 13, 14).* _Izingatiwe pia kwamba ilionywa kuwa watazuka watu wenye kufundisha kwa kufuata tamaa zao._
*(2 Timothy 4:3).* Kwa hiyo kwa wingi wao, wanadamu wanaweza kukosea.
Namna ya Kuikumbuka Sabato na Kuitakasa Kukumbuka na kuitakasa sabato ni kuelewa na kutekeleza kile ambacho Mungu anataka juu ya siku yake.
Mungu hajatuacha juu ya mwongozo kwa jambo hili.
SOMO lijalo tutajifunza kwa habari namna ya kuitunza Sabato
kupata masomo kama haya tembelea blog yangu inaitwa
π
https://masalianautume255.blogspot.com
MUNGU AKUBARIKI
0627729770(sms or call)
0712336509(whatsap)
__________Isack Mussa______
Bwana asifiwe mpendwa Msomaji wangu, nimekuwa nikitoa masomo mengi kwa habari ya Sabato.
basi kwa siku ya leo tutazichunguza kama zinae UKWELI wowote juu ya hili
sababu 11 watu waznazodai ya kwamba Sabato ilibadilishwa
*1. Je, tuheshimu Jumapili kwa kuwa Yesu alifufuka siku hiyo?*_ _Hapana._
Ni kweli baadhi ya wakristo wa awali kwenye miaka ya 90 hadi 100 BK walichagua kupumzika Jumapili kuepuka mateso makali yaliyowatofautisha na watu wengine.
Hata hivyo Yesu anadai Je, tukatae amri ya Mungu kwa kuheshimu mapokeo? Wanafunzi waliokutana Jumapili wengi hawakuamini kama Yesu amefufuka _(Mk. 16:12-14)._ Zaidi ya yote, mkutano wao wa Jumapili ulikuwa kwa hofu ya Wayahudi _(Yoh. 20:19)._
Yako maadhimisho mengine muhimu kama ubatizo na meza ya Bwana je na hayo tuyawekee siku gani?
*2. Je, si kalenda imebadilishwa?*
_Ni kweli kalenda ilibadilishwa mwaka 1582 lakini haikuingilia mzunguko wa juma lenye siku saba._
π Kilichobadilishwa na Papa Gregory XIII kilikuwa kusahihisha kosa kwenye kalenda ya Julian *(46 BC)* iliyosema mwaka una siku *365¼.* Kwa uhalisia kuna dakika 11 pungufu katika hesabu hiyo. Hadi mwaka *1582* , kulikuwa na upungufu wa siku 10. Hivyo, mwaka *1582* kulikucha Alhamisi 4 Oktoba *1582* na kesho yake kukawa Ijumaa tarehe *15* Oktoba *1582* .
_Tunapoabudu siku ya sabato tunafanya kama Yesu alivyoabudu._ *(Luka 4:16.)*
*3. Ni vigumu kutambua ni siku ipi ndiyo ya saba katika wiki.*
_Ziko sababu mbili kuhusiana na jambo hili._
Kwanza ni siku aliyokufa Yesu *Luka 23:52-56* kwamba alikufa Ijumaa na alifufuka Jumapili. *(Luka 24:1 – 2).*
Pili ni majina ya siku ya Jumamosi katika lugha mbali mbali zaidi ya 100 bado ni sabato.
π Italia, siku ya Jumamosi ni Sabbato, Hispania ni Sabado, Ureno ni Sabbado, Urusi ni Subbota, Poland ni Sobota na Ugiriki ni Sabbatho.
Maana ya majina yote hayo ni kwamba Jumamosi ndiyo sabato.
π Ikiwepo hoja ya tatu basi ni Kamusi. Ukisoma Kamusi, neno sabato, ni siku ya saba ya juma kwetu ni Jumamosi.
*4. Je naweza kutunza siku yoyote katika juma na kuiita Sabato?* _La:_
_Law. 10:1-2._ Wana wa Haruni walipoleta moto wa kigeni kwenye madhabahu, waliangamizwa papo hapo.
Hivyo, ni lazima kutakasa siku aliyoiweka Bwana mwenyewe. *(Kut. 20: 10.)* Zaidi ya yote, ukivunja amri moja, umekosa juu ya yote.
(somaπ *Yak. 2:10.*
Kwa miaka 40 yaani zaidi ya sabato 2000, Mungu aliwafundisha Israeli Sabato. (Kut. 16.) Kuokota siku 6, sabato hakipatikani na Ijumaa kiliokotwa kikahifadhiwa pasipo kuharibika. 5. Tutaitakasa siku ya Bwana, achana na Sabato *Ufunuo 1:9, 10* hutambulisha siku ya Bwana.
Siku za Bwana ziko nyingi. Malaki 4:1, 5 husema juu ya aina mojawapo na *Isaya 58:13* husema juu ya Sabato.
Yesu alisema ndiye Bwana wa Sabato. *(Mk. 2:28.).* Siku ya sabato humtambulisha Mungu kuwa Muumbaji na mkombozi na ndio maana uzito umewekwa kwamba tuikumbuke siku ya sabato tuitakase. (Kut.20:8).
*6. Sabato ilifanyika kwa ajili ya Wayahudi peke yao.*
π _Kuna uwongo wa kutisha ulioenea duniani kwamba sabato ni ya Wayahudi._ Lakini ndani ya Biblia wazo hilo haliungwi mkono.
Sabato inayoungwa mkono, ni _sabato ya Bwana._ *Kut. 20:10,* Ni kweli lipo sinagogi la Wayahudi. ( Mdo10:22, 12:11, 10:39 na 14:1.) Lakini sabato ni ya Bwana Kut. 20:10, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu π *Mk. 2:27.*
_Hivyo, kila aliye mwanadamu, sabato ni kwa ajili yake._
Luka ambaye hakuwa myahudi alitakasa sabato *(Mdo. 16:13.)* Na waongofu waliabudu siku ya Sabato *(Mdo. 14:42 – 44).*
*7. Amri 10 zilibatilishwa ikiwemo sabato.*
_Inaumiza moyo kwamba wako watu wanaolisema jambo hili pasipo kuungwa mkono na Maandiko Matakatifu._
Paulo anasema, kama isingekuwapo sheria, pasingekuwa na dhambi wala kusingekuwepo haja ya mwokozi. *Rum. 4:15.*
πSheria ya Mungu yote, pamoja na sabato ni ya haki, takatifu na njema
*Rum. 7:12.* _Sheria ya Mungu huwakilisha tabia ya Mungu._
*SHERIA ZA MUNGU NA NI MWAKISIO WA TABIA YA MUNGU*
*Rum 16:26 Mungu wa milele*
Zab. 111: 7,8 _Sheria ni ya milele_
*Luk.18:19 Mungu ni mwema*
_Rum. 7:12 Sheria ni njema_
*Yoh. 4:24 Mungu ni wa kiroho*
Rum.7:14 _Sheria ni ya kiroho_
*Kumb. 32:4 Mungu ni wa haki*
Rum. 7:12 _Sheria ni ya haki_
*Zab. 145:17 Mungu ni wa haki*
Zab.119:172 _Sheria ni ya haki_
*1 Yoh. 3:3 Mungu ni safi*
_Zab. 19:8 Sheria ni safi_
*Mt. 5:48* _*Mungu ni mkamilifu*_
*Zab. 19:7* _Sheria ni kamilifu_
*1Yoh. 4:8* *Mungu ni pendo*
Rum. 13:10 _Sheria ni pendo_
1 Yoh. 1:5 Mungu ni nuru
Mith. 6:23 Sheria ni nuru
Zab. 48:1 Mungu ni mkuu
Hos. 8:12 Sheria ni kuu
Kumb. 32:4 Mungu ni Kweli
Zab. 119:142 Sheria ni kweli
Isa. 5:16 Mungu ni mtakatifu
Rum. 7:12 Sheria ni takatifu
Kwa kuwa sheria ya Mungu ni mwakisio wa tabia ya Mungu, kwa kadiri tabia ya Mungu isivyobadilika, basi sheria nayo haitabadilika.
Kama ingekuwa rahisi Mungu kubadilisha sheria yake, basi asingekubali Yesu kuja kufa msalabani kwa ajili ya wanadamu.
Juu ya sheria ya Mungu kutofautiana na kile kinachoitwa Sheria ya Musa,
Angalia somo la Sheria ya Mungu.
8. Sabato ilibatilishwa Ni kweli yako mafungu ya Biblia yanayosema sabato ilibatilishwa.
(Kol. 2:16, Gal. 4:10 and Rum 14:5)
Biblia ikisomwa kwa makini itafunua kwamba hizi ni sabato zinazohusiana na sikukuu.
Kufuatana na Mambo ya _Walawi sura ya 23:_ angalia hasa fungu la 37, 38 kwamba zilitolewa kama nyongeza na ndio maana Paulo alizipinga. Tofauti na Sabato ya siku ya Saba, hiyo ilikuwapo kabla ya dhambi
(Mwa.2:1-3). Mungu akaiweka kwenye sheria yake ya maadili yaani amri kumi (Kut.20:8-11). Ni alama ya Mungu kwa aliowaumba na kuwatakasa (Kut.31:17, 13; Eze.20:20, 12).
Yesu alipokuwako duniani aliiheshimu. (Luk.4:16, Mt.24:20) na kwa kuwa Kristo habadiliki (Ebr.13;8), itakuwa furaha yake watakatifu kuabudu mbele zake siku za sabato, kwenye mbingu mpya na nchi mpya. (Isa.66:22, 23).
*9. Tuko chini ya neema hivyo hatulazimiki kutii sheria.*
*Rum. 6:14 – 15* _, Paulo anasema kwamba kwa kuwa chini ya neema, hatubatilishi sheria (Rum. 3: 31, Rum. 3:20.)_
*10. Tukiwa ndani ya Kristo, pumziko linatosha hivyo hatuihitaji sabato.*
_Ni Mungu ndiye atoaye raha hata kwa kupitia sabato yake. “Iko raha ya sabato kwa watu wa Mungu” (Ebr. 4:1-5, 9, 10)._
*N:B*
_Jinsi wokovu ulivyo muhimu kwa mwanadamu, *(Yoh. 3;16)* ndivyo sabato ilivyo muhimu kwa wanadamu. *(Mk.2:27)*_
*11. Watu wengi hawawezi kuwa wamekosea Wingi si hoja, bali ubora wa tabia ndio Mungu anaoutaka.*
*(Mt. 7: 13, 14).* _Izingatiwe pia kwamba ilionywa kuwa watazuka watu wenye kufundisha kwa kufuata tamaa zao._
*(2 Timothy 4:3).* Kwa hiyo kwa wingi wao, wanadamu wanaweza kukosea.
Namna ya Kuikumbuka Sabato na Kuitakasa Kukumbuka na kuitakasa sabato ni kuelewa na kutekeleza kile ambacho Mungu anataka juu ya siku yake.
Mungu hajatuacha juu ya mwongozo kwa jambo hili.
SOMO lijalo tutajifunza kwa habari namna ya kuitunza Sabato
kupata masomo kama haya tembelea blog yangu inaitwa
π
https://masalianautume255.blogspot.com
MUNGU AKUBARIKI
0627729770(sms or call)
0712336509(whatsap)
__________Isack Mussa______
Comments
Post a Comment