FAIDA 07 ZA MAOMBI YA KUFUNGA

Kujifunza zaidi kweli mbalimbali za Biblia
  Tembelea blog hii hapa

            https://masalianautume255.blogspot.com/

FAIDA 07 ZA MAOMBI YA KUFUNGA

         Kwa neema ya MUNGU naona Mungu anakwenda kutenda kitu juu yako unapokwenda kuusoma ujumbe huu wote

Usisahau kushare angalau magroup 5 uliyonayo ili tuweze kushiriki baraka hizi

Soma ujumbe huu wote utaona nguvu iliyopo katika Maombi ya kufunga na kuomba

1.Hufungua hekima ya kupokea Maombi kwa Mungu

Tunapohitaji hekima za Mungu, akili zetu zijishughulishe kwa mambo ya kiroho
(yakobo 1:5)

2.huisha kupokea/kufufua mambo ya kiroho .

Hatuwezi kuwa watakatifu kama Hatuwezi kufunga na kuomba, jipangie ratiba ya Maombi ya kusali na kufunga hata kwa vikundi

3.kuamsha Ari (shauku) ya kujenga tabia kama ya Yesu

Hatuwezi kuwa na tabia ya Yesu hata siku moja kama hatufungi na kuomba,  na Mungu atakufanya uwe kichwa na sio mkia

Wewe Muadventista Msabato unapaswa kufunga na kuomba ili tuzidi kuiga tabia ya Yesu

Ili tuzidi kuipata ile subira ya watakatifu
(ufunuo 14:12)

Laiti wote wangaecha ibada ya Sanamu na kutii amri za Mungu na
wangefunga na kuomba Basi hata *KORONA* ingeisha

Watu leo wamekuwa wakaidi wanavunja Sheria ya Mungu  ndio maana hata KORONA imekuwa ni janga kubwa

Ibada ya Miungu
Ibada ya Sanamu
Ibada ya Jua (sun day)

Ulimwengu wote ungeamua kutii tu amri zote 10 hakika hata KORONA tungemuomba Mungu Mara moja tu na angeiondoa ndani ya dakika moja isiwapo tena ulimwenguni

Wakati mwingine tunakumbana na Majanga mbalimbali Kwasababu hatutii Amri zake Mungu pamoja na ibada ya Sabato

Jiulize kwanini ushike amri 9 tu halafu hiyo moja ikufanye uhesabiwe umezivunja amri zote

4.Hufungua hazina ya ile Kweli ya Mungu
(2 petro3:16)

Wengi husoma Biblia kama Gazeti lakini kwa kufunga na kuomba wote tungekuwa na tafsiri moja na Dini moja tu Ulimwengu wote

Unaweza kuwa Msomi mzuri wa BIBLIA lakini ukawa mpotoshaji Kwasababu hekima ya kulisoma Neno la Mungu haipo ndani yako,  na ndio maana wengi leo wanaipotosha Biblia kwa kuhafifisha ujumbe wa Malaika watatu

Naweza kusema hili maana hata makanisani mwetu nyimbo za Unabii wa Danieli na Ufunuo zimepungua

Hii ni hila ya Shetani amewafanya watakatifu wasisome Unabii wa Danieli na Ufunuo.

Wainjilisti wanasambaza vitabu tunanunua lakini hatuvisomi Kwasababu wengi hatufungi na kuomba

5.Huandaa watu wa Mungu kwa kazi ya Mungu
(Matendo 13:1-3)

Ninaomba kuanzia leo tujiwekee ratiba ya Maombi ya kusali na kufunga

Hata Yesu alipokuwa nyikani alifunga na kuomba kwaajili ya mpango wa kumkomboa Mwanadamu

Hivyo hata sisi tukifunga na kuomba tutaweza kuwaokoa walio gizani,  kuwaponya wagonjwa na wenye shida mbalimbali

Nataman sana siku ya leo watakatifu wa Mungu tuwe na Maombi ya kusali na kufunga mambo mengi yatawekwa wazi

6.Huyashinda majaribu na Mateso

Umeteseka na kujaribiwa,  dawa ni kuingia katika Maombi ya kusali na kufunga

Kumbuka kila kisa cha Esta Malikia (Esta 4:16)

Kumbuka Petro alipofungwa gerezani kanisa lilifunga na kuomba

Petro gerezan ile minyororo ilifungukwa kwaajil ya Maombi ya kufunga

milango ya chuma ilifunguka yenyewe.
(matendo 12:5,12).

Huenda leo upo katika Gereza nene kama vile :-

Gereza la  Maandiko.
Akili yako imefungwa unayafasiri Maandiko vibaya

Gereza la magonjwa
Gereza la kutotii Amri za Mungu
Gereza la uzinzi
Gereza la kutotii Sabato n.k

Mungu leo atafungua Gereza lako utakapokwenda kufunga na kuomba


2 mambo ya nyakati 7:14

14 _ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao._

7.huwatayarisha watu wa Mungu kwa siku za mwisho

tunaishi katika kipindi cha mwisho na hatima inakwenda kutimia., angalia usije ukawa ni mpashaji joto wa viti kanisani Kwasababu hiyo nafasi yako itachukuliwa na mwingine,  hivyo kuwa makini.  twapaswa kufunga na kuomba, na kutafakari neno lake

twapaswa tuwe na kina kutafuta mambo ya Mungu, kila mmoja twapaswa kuwa na ratiba ya kuomba

dhiki iliyo mbele yetu watakaoweza kushinda ni wale wenye kufunga na kuomba maana ndio watakaokuwa imara katika kumwabudu Mungu kwa Roho na Kweli

siku inakuja watakatifu watalia na kusaga meno ila tukimtegemea Mungu hatutayumbishwa Kwasababu mbele lipo tumaini

Naona hatari kubwa inayokuja mbele yetu na Moyo wangu unanishuhudia niyaseme haya ili kila mwenye sikio ayasikie na aweze kirekebisha njia zake

Kwa imani hivi leo anza kufunga na kuomba.

Katika Maombi yako usisahau kuomba haya
👇👇
1. Mungu akuonyeshe Sabato ya Kweli ni ipi

2.Omba Roho Mtakatifu akufundishe kuyajua Maandiko Matakatifu maana wengi wameyapotoa Kwasababu hawajamruhusu Mungu awafundishe

3. Omba Mungu akuonyeshe Kanisa la Kweli ambalo limebeba sifa hizi

(ufunuo 14:12)
(Isaya 8:20)

Mungu akubariki sana unapokwenda kufanya Maombi haya.

By
Isack Mussa
                         0627729770 au
0689980058

Comments