kwa Nje Wengi wanashawishika kufikiri kwamba wao wako katika njia ile iendayo mbinguni ati kwa sababu tu wanakiri kumwamini Kristo, wakati wanaikataa Sheria ya Mungu [Amri Kumi].
Lakini hao watagundua mwishoni kwamba walikuwa katika njia ile iendayo kwenye uharibifu badala ya ile iendayo mbinguni. Sumu ya kiroho inapakwa sukari kwa nje kwa njia ya fundisho [potofu] la utakaso, na kuwapa watu waimeze. Maelfu kwa hamu kubwa huimeza, wakijisikia ya kwamba ikiwa wao ni waaminifu tu katika imani yao hiyo, basi, watakuwa salama.
Lakini uaminifu huo hautaweza kamwe kuligeuza kosa [fundisho potofu] kuwa kweli.
Mtu anaweza kumeza sumu, akidhani kwamba ni chakula; lakini uaminifu wake [katika kuamini hivyo] hautaweza kumwokoa kutokana na madhara ya sumu hiyo aliyoimeza.
Mungu ametupa sisi Neno lake kuwa kiongozi wetu. Kristo amesema, "Mwayachunguza [Chunguzeni] Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia" (Yohana 5:39, KJV). Aliwaombea wanafunzi wake, akisema, "Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli" (Yohana 17:17). Paulo asema hivi, "Kweli, mimi mwenyewe naliona ndani ya nafsi yangu kwamba yanipasa kutenda mambo mengi yaliyopingamana na jina lake Yesu Mnazareti" (Matendo ya Mitume 26:9). Lakini imani hiyo haikuifanya njia yake iwe ya kweli.
👇
Paulo alipoipokea injili ya Yesu Kristo, ilimfanya kiumbe kipya. Alibadilika kabisa; kweli iliyopandwa moyoni mwake ilimpatia imani ile na ujasiri ule aliokuwa nao kama mfuasi wake Kristo hata upinzani wo wote ule haukuweza kumtikisa, wala mateso kumtia hofu.
👇👇
Watu wanaweza kutoa udhuru wo wote wanaotaka kama sababu ya kuikataa Sheria ya Mungu [Amri Kumi]; lakini hakuna udhuru wo wote utakaokubaliwa katika siku ile ya hukumu [ambayo inaendelea hivi sasa huko mbinguni].
👉 Wale wanaoshindana na Mungu na kuzitia nguvu nafsi zao zenye hatia kwa kuendelea kuivunja Sheria ya Mungu [Amri Kumi], hivi punde watalazimika kukabiliana na Mtoa-Sheria Mkuu juu ya Sheria yake iliyovunjwa [Amri Kumi]. Siku ya kisasi cha Mungu yaja ---- siku ile ya ghadhabu yake kali sana. Ni nani atakayesimama [atakayestahimili] siku ile ya kuja kwake? Wanadamu wameifanya mioyo yao kuwa migumu kwa kumpinga Roho wa Mungu, lakini mishale ya ghadhabu yake itapenya mpaka ndani ya mioyo yao mahali pale iliposhindwa kupenya mishale ile ya kuwathibitishia dhambi zao.
👉Si mbali kuanzia sasa Mungu ataondoka kuja kumshughulikia mwenye dhambi [yule asiyetaka kutubu]. Je! yule mchungaji wake wa uongo atamkinga mvunja sheria [Amri Kumi] huyo siku ile?
Je. ! anaweza kusamehewa yule aliyeandamana na mkutano katika njia ile ya uasi? [ _Kutoka_ 23:2]. Je! kule kupendwa [Je! anaweza kusamehewa yule aliyeandamana na mkutano katika njia ile ya uasi? [Kutoka 23:2]. Je! kule kupendwa [kwa fundisho hilo potofu] na watu wengi au idadi kubwa [ya waumini] kutaweza kumfanya mtu ye yote asiwe na hatia? Haya ndiyo maswali ambayo wale walio wavivu na wasiojali [kusoma Neno la Mungu kujua linavyosema juu ya Sheria yake] wanapaswa kuyatafakari na kukata shauri wao wenyewe juu ya kile watakachofanya. SURA YA 3 Kristo Ni Haki Yetu fundisho hilo potofu] na watu wengi au idadi kubwa [ya waumini] kutaweza kumfanya mtu ye yote asiwe na hatia? Haya ndiyo maswali ambayo wale walio wavivu na wasiojali [kusoma Neno la Mungu kujua linavyosema juu ya Sheria yake] wanapaswa kuyatafakari na kukata shauri wao wenyewe juu ya kile watakachofanya. SURA YA 3 Kristo Ni Haki Yetu.
*
Usikose kutazama video hii you tube
Mapigo saba baada ya Sheria ya Jumapili kupitishwa
* 👇
*https://youtu.be/YNypV-79ik8*
MUNGU AKUBARIKI
Isack Mussa
_Kwa Mawasiliano_
*0627729770*
*0712336509*
Comments
Post a Comment